Mbunge mteule wa jimbo la Nzega, Hamisi Kigwangalla ameukejeli Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kupinga mwenendo wa Tume ya Taifa katika zoezi la kutangaza matokeo ya urais kutoka majimboni.
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Kigwangalla ameeleza kuwa Ukawa wamefanya majumuisho na kugundua kuwa wameshindwa katika uchaguzi wa mwaka huu hivyo wameanza kulalamika.
MaUKAWA yamejumlisha kura yameona yameshindwa, hayaamini, yameanza kulialia – #DenialState (in psychology). Taratiibu watakubali tu!
— Hamisi Kigwangalla (@HKigwangalla) October 28, 2015