Walipa Kodi nchini wametakiwa kulipa Kodi kwa wakati na kwa kiwango kinachostahili kulipwa kwa ni Serikali inatoa huduma za kijamii kutokana na kodi hizo.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Salum Ali Hapi alipotembelea Ofisi za Mamlaka ya Kodi Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi wa Kinondoni leo Jijini Dar es Salaam.

Hapi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais, Magufuli katika vipaumbele vyake ni pamoja na kuhakikisha watu wanaostahili kulipa Kodi wanalipa kwa wakati kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Aliongeza kuwa ili Serikali kutimiza haki ya utoaji wa huduma za msingi ni lazima watu walipe Kodi.

“  TRA hakikisheni kila anayestahili kulipa Kodi analipa kwa wakati na kiwango stahiki, kwani Serikali inaendeshwa kwa Kodi, Elimu bure,huduma za Afya , maji na mengine chanzo ni kodi” Alisema Hapi.

Serikali itatoa ushirikiano wowote utakaohitaji ili kusaidi udhibiti wa wakwepa kodi kupitia vyombo vya dola na mamlaka zingine ili kusafikisha azma ya kila anayestahili kulipa kodi alipe kwa wakati bila kujali ni nani.

Aidha alitoa ushuri kwa uongozi wa Mamlaka hiyo kuboresha mfumo wa utoaji wa huduma kwa wateja wao ili kuondoa malalamiko yasiyo ya msingi.

Kwa upande wake Meneja wa TRA, Mkoa wa Kikodi wa Kinondoni, Wallace Mnkande amesema kuwa wamevuka lengo la ukusanyaji wa mapato kwa zaidi ya shilingi bilioni 3 ambapo jumla ya shilingi bilioni 43 zimekusanywa kwa mwezi Agosti huku lengo likiwa ni shilingi bilioni 40.57.

Meneja huyo ameongeza kuwa TRA Kinondoni wamejipanga kuhakikisha wanaongeza ukusanyaji wa Kodi ili kuvuka malengo zaidi kwani ni eneo ambalo linawalipa kodi wengi na wakubwa.

Katika kurahisisha utendaji wa majukumu TRA Kinondoni imegawa ofisi zake katika kanda nne ambazo ni Tegeta, Manzese, Kimara na Millenium Tower kwa ajili ya walipa kodi za Leseni za Madereva

Video: DC Hapi afanya ziara ya kushtukiza TRA
Mwisho Wa Kujisajili GPX Ni Jumatatu