Kesi ya mtuhumiwa wa kigaidi Brenton Tarrant, aliyewauwa watu 51 na kujeruhi wengine 49 katika shambulizi  la silaha kwenye misikiti miwili huko Christchurch, New Zealand, imeanza kusikilizwa.

Mtuhumiwa huyo anatarajiwa kuhukumiwa kifungo cha maisha baada ya siku 4 za mashtaka,ambapo kesi hiyo inatarajiwa kudumu kwa siku 4, chini ya hatua kali za usalama.

Tarrant atakayehukumiwa na jaji wa Mahakama Kuu ya Christchurch, Cameron Mander, atahudhuria kusikilizwa kwake kupitia mfumo wa video na sauti kutoka Gereza la Auckland ambapo ameshikiliwa.

Hata hivyo Tarrant, ambaye ombi lake la kujitetea lilikubaliwa na Mahakama Kuu ya Christchurch mnamo Julai 13, alikuwa amekubali mashtaka yote dhidi yake, pamoja na mauaji 51, majaribio 40 ya mauaji, na shambulizi moja la kigaidi.

Ikumbukwe Tarrant alishambulia msikiti wa Nur na Linwood kwa silaha huko Christchurch wakati wa sala ya Ijumaa mnamo Machi 15, 2019, ambapo watu 51, mmoja wao akiwa ni raia wa Kituruki, walipoteza maisha na watu 49 walijeruhiwa, wakiwemo Waturuki wawili.

Wajawazito kuendelea na masomo Zimbabwe
Young Africans yawaalika mabingwa wa Burundi