Kocha wa Simba, Fadlu amewagomea FAR Rabat ya Morocco juu ya dili la kutaka kumng’oa Msimbazi, akiwaambia hataki kuifanyia ‘ubaya ubwela’ Simba inayopigania mataji muhimu hivyo kama wanamhitaji siriazi basi wasubiri msimu umalizike.
Jibu hilo la Fadlu likawafanya FAR Rabat kufanya uamuzi wa haraka kumchukua chaguo lao la pili Mreno Alexander Santos, ambaye ni kocha wa zamani wa CS Sfaxien na Petro Luanda ya Angola.
Hadi jana Santos alibakiza mambo machache kutambulishwa kuwa kocha mpya wa timu hiyo ya Jeshi la Mfalme wa Morocco ambayo msimu uliopita ikiwa chini ya Nasreddine Nabi aliyepo Kaizer Chiefs ya Sauzi, iliukosa ubingwa wa Botola Pro mbele ya Raja Casablanca aliyekuwapo Fadlu kama kocha msaidizi.