Mashambulizi baina ya Israel na Palestina yamesimamishwa, baada ya siku 11 za ghasia kati ya pande hizo mbili.

Israeli imeukubali mpango wa Misri wa kusitisha mapigano mabaya zaidi kuwahi kutokea tangu mwaka 2014, na imekubali bila masharti yoyote.

Misri sasa inatarajiwa kutuma wajumbe nchini Israeli na Ukanda wa Gaza katika siku chache zijazo kwa lengo la kuumaliza kabisa mgogoro huu.

Maafisa wa Hamas wanasema huenda makubaliano ya sasa yakawa na nguvu iwapo tu Israel itaacha kutumia nguvu katika masuala ambayo yanahitaji diplomasia, huku Israel ikisema Hamas inahitaji kushauriana vyema na mamlaka ya Palestina ili kunusuru machafuko mengine.

Nchi kadhaa zimehusika katika majadiliano hayo ya muda mrefu ikiwemo Misri, ambayo ni mshirika wa karibu wa pande zote mbili kwa sasa.

Rais wa Marekani Joe Biden amesema mazungumzo ya siku 11 yamesaidia kufikia mafanikio hayo.

Kaizer Chiefs wajihami mapema
Habari kubwa kwenye magazeti leo, Mei 21, 2021