Msajili wa vyama vya siasa  Jaji Francis Mutungi amewataka waandishi wa habari kusaidia kuwaondoa hofu wananchi kuhusu hofu na taharuki inayoendelea kujengeka kuhusu uvunjifu wa amani pasipo msingi  katika mandamano yanayotarajiwa kufanywa baadhi ya vyama vya siasa Agosti 31 na septemba mosi mwaka huu.
Hayo  yamesemwa leo na msajili wa vyama vya siasa nchini jaji Francis Mutungi  jijini Dar es salaam,alipokuwa akiongea na waandishi wa habari na kuongeza kuwa wananchi wasiamini kuwa  kuna ombwe la kiutendaji na kubaki njiapanda kwamba hakuna njia ya kufikia  suluhu au kupata muafaka katika mambo yanayo endelea katika duru za siasa hapa nchini.

Aidha amewaomba  wadau wote na  vyama vya siasa wanaoitisha maandamano kuwa na subira na kufanya mazungumzo kwa kuwa anaamini katika mazungumzo muafaka utapatikana,na utawala bora ni pamoja na kuheshimu taratibu zilizopo.

Pamoja na hayo Mutungi amesema baraza la siasa litafanya vikao mfululizo tarehe 29 na 30  mwezi huu na kikao hicho kitakuwa maalumu kwa mazungumzo kwaajiri ya kutafuta kufikia suluhu ya jambo hilo la maandamano.

Wapenzi Wa Jinsia Moja Wajifungua Watoto Watatu Afrika Kusini
Polisi Wazuia Msafara Wa Lowassa, Wakwama Kuelekea Mikoa Ya Katavi Na Rukwa