Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Rehan Baig (37), raia wa Uingereza amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kosa la kufanya mapenzi na kuku hadi kufa .

Tukio hilo lilitolewa ushahidi na mfanyakazi wa ndani pamoja na kamera ambazo zilinasa picha na video za jamaa huyo akifanya kitendo cha udhalilishaji kwa kuku huyo aliyekuwa na rangi ya kahawia na nyeupe.

Mahakama ya ‘Bradford Crown Court’ ambayo imetoa hukumu hiyo kupitia Jaji wake amesema kuwa kitendo cha tabia hiyo ni cha upotoshaji na udhalilishaji, kwani mnamo Julai 9,2020 alikutwa na picha za unyanyasaji wa kingono kwa watoto.

Licha ya kuhukumiwa miaka mitatu gerezani, pia amepigwa marufuku ya kutojihusisha na masuala ya wanyama na ndege kisha jina lake limeingizwa katika orodha ya watu wahalifu wa kingono wa maisha.

Kaze: Viungo wanaiangusha Young Africans
Guinea: Alpha Conde aongoza matokeo ya awali