Maafisa wa Polisi wapatao 1,000 wamesimamishwa kazi na wengine kuwekewa masharti katika majukumu yao, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kulisafisha Jeshi la Polisi la mji mkuu wa London, linalokabiliwa na kashfa.

Kikosi hicho, ambacho ni kikubwa nchini humo kimekabiliwa na mlolongo wa kashfa ambazo zimedhoofisha imani ya raia kwa Polisi wa Uingereza.

Kashfa hizo, zinajumuisha ubakaji na mauaji ya msichana aliyechukuliwa kimabavu barabarani na afisa mmoja wa Polisi.

Kwa mujibu wa Polisi, kati ya maafisa 34,000, 201 kati yao wamesimamishwa kazi na takriban 860 hawaruhusiwi kufanya baadhi ya shughuli.

Ripoti: Zaidi ya Watoto 1,200 wadaiwa kufariki Dunia
Habari Kuu kwenye magazeti ya leo Septemba 20, 2023