Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amewataka mawaziri wote pamoja na makatibu katika wizara kuchukua likizo ya mapumziko ya lazima huku kukiwa na taarifa za mabadiliko kwenye baraza la mawaziri.

Rais Kenyatta amesema kuwa mawaziri na makatibu watalazimika kushughulikia majukumu ya dharura.

Kwa mujibu wa barua iliyotumwa na mkuu wa utumishi wa umma Joseph Kiyua likizo hiyo ya siku 11 itaanza Agosti 17 hadi agosti 28, mwaka huu ambapo mawaziri hawatafanya ziara za kukagua miradi na mipango ya serikali.

Likizo hiyo ya mawaziri na makatibu inakuja huku kukiwa kuna taarifa kuhusu Rais Kenyatta kuifanyia mabadiliko baraza la mawaziri.

Fahamu aina za wateja wa kuwaepuka kwenye biashara
R.Kelly atuhumiwa kuwatishia maisha waliomshtaki