Mwanahabari na mchambuzi wa mchezo wa kabumbu hapa nchini , Hemed Kivuyo ,Amesema kuwa vilabu vinatakiwa kutokutegemea uzamini wa ligi pekee, bali kutafuta uwekezaji zaidi.

akizungumza na Dar 24 , Kivuyo amesema kuwa suala la uwekezaji kwa vilabu ni mwarobaini wa kiuchumi .

“ushindani utakuwa mkubwa sana isipokuwa baadhi ya timu ambazo hawana uwekezaji na gharama zao ni ndogo kiukweli navyoona wataendelea kusota sana,” amesema Kivuyo .

Kivuyo amesema kuwa pamoja ligikuwa na udhamini vilabu havitakiwi kutegemea pesa hiyo kwakuwa ni ndogo sana kwenye uendeshaji wa klabu, “klabu inapaswa ijitavutie wadhamini na kuachana na ule wa ligi , wajibrand,kitengo chao cha masoko kiwe bora muda wote na wahakikishe wanapata udhamini,”.

vilabu vya soka vinaendelea na maandalizi ya mwisho kuelekea ligi kuu Tanzania bara inayotarajiwa kuanza jumamosi ya Septemba 5 .

Bofya hapa ….

Platini kitanzini tena
Neville atoa ushauri wa bure Manchester United