Aliyekuwa Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea amefikishwa mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na kuachiwa kwa dhamana leo Septemba 11, 2020.

Kubenea anatuhumiwa kuingiza fedha za kigeni bila kutoa tamko na kuingia nchini kinyume cha sheria ya uhamiaji.

Kubenea alikamamatwa na polisi Septemba 7, mwaka huu akiwa katika gari la abiria lenye namba ya usajili T. 645 DKR akitokea kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea Arusha mjini.

Kesi inayomkabili itatajwa tena Sepetemba 21 mwaka huu.

Yaliyowakuta Clouds yahamia Wasafi
Wazo la kujiua ni dalili za ugonjwa wa akili