Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema kuwa baraza jipya la mawaziri lililotangazwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli halina jipya kwani sura zilizobaki ni zile zile.

Ameyasema kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa Twitter, ambapo amesema kuwa ameona mabadiliko ya baraza la Rais Magufuli lakini bado fikra ni zile zile na watu ni wale wale na kudai katiba mpya ndio suluhisho la vyote.

“Nimeona Mabadiliko ya baraza la JPM. Watu ni wale wale, fikra zile zile. Katiba Mpya yenye fikra mpya ndio tumaini kwa mabadiliko sahihi ya nchi na watanzania kwa ujumla,”ameandika Lema

 

 

Nelly akamatwa kwa tuhuma za ubakaji
Bafana Bafana yaichapa Burkina Faso Uganda ikitoshana nguvu na Ghana