Ratiba ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Novemba 26, 2017, katika vituo viwili vya majiji ya Dar es Salaam na Arusha, imetangazwa.

Katika ratiba hiyo, Kundi A limepangwa kuwa katika Kituo cha Dar es Salaam ambako timu zake Simba Queens ya jijini Dar es Salaam iliyopanda daraja msimu huu, Mburahati Queens, JKT Queens, Evergreen zote za Dar es Salaam pamoja na timu za Fair Play ya Tanga na mabingwa watetezi – Mlandizi Queens.

Kundi B litakuwa na timu za Alliance ya Mwanza ambayo imepanda kutoka kituo cha Dodoma. Timu nyingine ni Marsh Academy pia ya Mwanza; Panama ya Iringa; Kigoma Sisterz ya Kigoma, Baobab ya Dodoma na Majengo Queens ya Singida.

Fungua dimba kwa Kituo cha Dar es Salaam, mabingwa watetezi wa taji hilo, Mlandizi Queens itacheza na JKT Queens katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.

Katika kundi hilo la A, mechi nyingine zitakuwa siku inayofuata Novemba 27, mwaka huu kati ya Mburahati Queens na Evergreen saaa 8.00 mchana wakati Fair Play ya Tanga itacheza na Simba Queens saa 10.00 jioni.

Jijini Arusha, Panama ya Iringa itafungua dimba na Alliance Queens ya Mwanza huku siku ya pili Novemba 27, mwaka huu Baobab Queens itacheza na Marsh Academy saa 8.00 mchana wakati saa 10.00 jioni Majengo Queens itapambana na Sisterz ya Kigoma.

Timu hizo zitapambana katika vituo hadi Desemba 12, mwaka huu kabla ya kutoa jumla ya timu nane kwa maana ya nne kutoka kila kundi. Timu hizo nane zitapambana katika hatua ya Nane Bora ya Ligi hiyo kuelekea ubingwa. Ligi inatarajiwa kumalizika Machi 28, mwakani.

Ummy Mwalimu apiga marufuku biashara ya damu
TFF yatoa ufafanuzi wa malipo ASFC