Kwa mujibu wa wataalamu wametoa maelezo mafupi juu ya maana sahihi ya hedhi na kusema kuwa ni kipindi maalumu katika mzunguko wa mwanamke mwenye umri wa kuzaa. Wakati huo, ambao kwa kawaida unarudi kila baada ya mwezi mmoja kwa  kutokwa na damu kwenye uke.

Ni vyema kufahamu mambo kadhaa hasa yanayohusu masuala ya afya ambayo muda mwingine tunaweza kuwa tunayafanya bila kutambua madhara yake.

Madaktari katika tafiti zao walichambua baadhi ya madhara kwa mwanamke na mwanaume kushiriki tendo wakati wa hedhi.

Ambapo kwa upande wa mwanaume takribani madhara 6 yaliweza kuainishwa yakiwemo.

  1. Kupata maambukizi katika njia ya mkojo hadi kwenye kibofu
  2. Maambukizi katika tezi dume, hii inaweza kuathiri mfumo wa uzazi wa mwanaume.
  3. Kuziba kwa njia ya mkojo
  4. Utasa au ugumba
  5. Ulegevu wa misuli ya uume na upungufu wa nguvu za kiume
  6. Athari mbaya ya kisaikolojia kwa kufanya tendo katika mazingira yasiyo safi hali inayoweza kupelekea kutolifurahia.

Lakini pia madaktari hao waliweza kuainisha athari za kushiriki tendo kwa mwanamke aliye mwezini.

  1. Kupata maambukizi katika viungo vya ndani vya uzazi kama vile shingo ya kizazi, mirija ya uzazi kwa ujumla anaweza kupata matatizo na kuathiri mfumo wake wa uzazi
  2. Maumivu makali ya tumbo hasa kwa wale wanaopatwa na maumivu wakati wa hedhi
  3. Utokali damu unaweza ukaongezeka kuliko vile inavyotoka kwa kawaida
  4. Utasa au Ugumba
  5. Kuvimba kwa kuta za ndani za uke kwa kuwa wakati wa hedhi zenyewe huwa tayari zimevimba kweney uke wakati wa tendo
  6. Mwanamke hiathirika kisaikolojia n akutokufarahia tendo.

CAG ahojiwa na kamati ya maadili ya bunge
Jaribio lingine la Al-Shabaab lazimwa Kenya, wakimbizwa