Mgombea Urais CCM ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli atachukua fomu wiki hii Dodoma akiomba dhamana kwa mara ya pili.

Hayo yamesema na naKatibu Itikadi na Uenezi CCM Humprey Polepole leo Agost 5, 2020 wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam.

Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika Agost 28, 2020 ambapo NEC imefungua zoezi la Uchuaji fomu ngazi ya Urais kuanzia leo na kuhitimishwa Agost 25, 2020.

”napenda kuwatangazia rasmi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli ambaye sisi kwenye chama chetu ndiyo muasisi mkubwa wa uwazi, atachukua fomu wiki hiini lini nitawaambia tena, lakini wiki hii mgombea CCM atachukua fomu kule Jijini Dodoma” amesema Polepole

Ikumbukwe Rais Magufuli alipitishwa Mkutano Mkuu wa CCCM kugombea nafasi hiyo Julai mwaka huu ambapo Rais Magufulia anagombea kwa mara ya pili baada ya kushinda Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015.

Tetesi: Aissa Mandi anukia Liverpool
Dybala mshindi wa MVP, amkandamiza Ronaldo