Hatimaye mapacha wanaounda kundi la P Square, Peter na Paul wametangaza kuzika rasmi tofauti zao na kurejea kama zamani.

Taarifa za kuzika bifu hilo zimetolewa na Peter ambaye awali alionekana kama ndiye aliyechangia kwa kiasi kikubwa kusambaratika kwa kundi hilo akiingia katika ugomvi na ndugu zake Paul na Jude ambaye alikuwa meneja wao kwa muda mrefu.

Kupitia Instagram, Peter amepost kipande cha video akiwataka mashabiki kumlaumu yeye kwa yote yaliyotokea na kwamba wameamua kudumisha udugu wao na kurejea katika usimamizi wa kaka yao, Jude Okoye.

“Nataka kuwajibika kwa yote yaliyotokea na nawaomba radhi kwa dhati mashabiki wetu. Kwa kutuunga mkono muda wote katika safari hii, mnatudai mengi ziadi ya yale tuliyowapa na ninaomba radhi kwa hilo. Tumerudi sasa katika safari mpya na usimamizi mpya (Jude Okoye), muziki mpya na mawazo mapya,” inaeleza sehemu ya ujumbe mrefu aliouandika Peter kwenye Instagram.

My dear fans, P-Square is back. Ours is a journey that started from our mother’s womb. It was a journey that started from Primary School, continued to St. Murumba College, to when we were in University in Abuja. It was a journey in which we shared childhood memories and grown-up dreams. We are back because brothers do not let each other wander in the dark alone. We are back because we have tried the lonely road and it was not the same. I want to take responsibility for what has happened and sincerely apologise to you our fans. For supporting us throughout this journey we owed you so much more than what you have had to endure and I apologise for that. We are embarking now on a new journey with exciting new management (Jude Okoye), new music and new ideas. We cannot thank you enough for all your prayers and support throughout this difficult period. Maya Angelou once said that brotherhood is a condition that people have to work at. We will continue to work on that and you can be prepared to be blown away by this new phase of P-Square. God bless you all and be assured that you have not seen anything yet! Peter Okoye P-Square

A video posted by Peter okoye (Psquare) MrP (@peterpsquare) on


Mapacha hao walikuwa katika ugomvi mkubwa kwa kipindi kirefu huku kila mmoja akitangaza kufanya kazi zake binafsi. Ugomzi wao ulikuwa gumzo katika tasnia ya muziki Afrika huku wasanii wakubwa kama 2 Baba Odibia wakieleza kuwa wamejaribu kuwapatanisha mara kadhaa lakini juhudi zao hazikuzaa matunda.

Video: Serikali Yazindua Program Ya Kumekucha
TANAPA Yaipiga Tafu Timu Ya Taifa Ya Riadha