Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amesema kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ameruhusu kuanza mchakato wa ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Ruhuji mkoani Njombe utakaozalisha megawati 358, kwa lengo la kuwa na hazina kubwa ya nishati ya umeme ambao utauzwa katika nchi jirani ikiwemo Zambia, Kenya na Uganda.
 
Ameyasema wakati akiwasha umeme katika vijiji vinne vinavyopitiwa na ujenzi wa mradi wa umeme wa Makambako -Songea ikiwa na pamoja na kijiji cha Ngalanga, Lyamkena, Ilembela na Magoda wilayani Njombe, ambapo amesema kuwa jitihada kubwa na maamuzi magumu yanayochukuliwa na serikali ya awamu ya tano katika ujenzi wa miradi mikubwa ya umeme zina lengo la kuwa na kiwango kikubwa cha nishati ambayo itaweza kuuzwa nchi jirani zenye uhitaji.
 
Amesema kuwa serikali imepanga ifikapo mwaka 2020 vijiji vyote elfu 12 vya Tanzania viwe vimewashwa umeme na hivyo kufungua milango kwa watalaamu binafsi wenye ujuzi wa kuzalisha umeme kuanza kutumia ujuzi wao kuanzisha miradi kwa manufaa ya taifa.
 
“Tayari serikali yetu ina mpango wa kuanzisha mradi mkubwa wa umeme katika maporomoko ya mto Ruhuji hapa Njombe, hizi ni jitihada kubwa zinazofanywa na raisi wetu Dkt. John Pombe Magufuli na sisi kama wizara ya nishati tupo pamoja naye katika kuhakikisha mipango hii inafanikiwa kwa haraka,”amesema Mgalu.
 
Naye mbunge wa jimbo la Njombe Mjini kupitia CCM, Edward Mwalongo amesema kuwa kila mwananchi anapaswa kutumia fursa hiyo kujisajili kwa gharama nafuu kabla gharama halisi hazijaongezwa huku akisikitishwa na wanaobeza jitihada zinazofanywa na Serikali katika kusogeza huduma kwa wananchi.
 
Kwa upande wao wananchi wa vijiji hivyo ambavyo vimepata umeme kupitia mpango wa REA wamesema kuwa ujio wa nishati ya umeme katika vijiji vyao utakuza uchumi kwa kasi kwa kuwa kumekuwa na viwanda na mashine ambazo wakati mwingine zinashindwa kufanya kazi kwa kuwa zinatumia mafuta.
 
  • Makonda anena makubwa mbele ya JPM, ‘2020 kitaeleweka tu’
  • Ndani ya vyama vya upinzani kuna mapungufu- Halima Mdee
  • LIVE: Rais Magufuli akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja jipya la Salenda
 
Zaidi ya vijiji 120 vinavyopitiwa mradi mkubwa wa Makambako -Songea vipo kwenye mpango wa kuwashwa umeme ikiwa ni utekelezaji wa mpan

RC Gaguti atekeleza agizo la JPM
Makonda anena makubwa mbele ya JPM, '2020 kitaeleweka tu'