LG imefanya kweli tena baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Ukanda wa Afrika Mashariki, Dongwon Lee kungoza watendaji na wafanyakazi wa kampuni hiyo katika Semina ya Mawakala (Dealers Seminar) ya aina yake Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine mawakala hao walipewa mafunzo maalumu kuhusu teknolojia mpya za LG na baadaye wakashiriki katika kipindi cha maswali na majibu ambapo washindi walijinyakulia zawadi mbalimbai za kusisimua kutoka LG.

Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Balozi wa Korea nchini Bw KIM, Sun Pyo na Balozi wa India nchini Bw Binaya Srikanta Pradhan.

Polepole awasilisha hati za ubalozi Havana - Cuba
Mume alalama kunyimwa unyumba, kupigwa na mkewe