Mkurugenzi wa Shirika la Ndege nchini (ATCL), Mhandisi Ladislaus Matindi amekanusha taarifa kuwa, ndege ya Dreamliner 787-8 ina hitilafu na kwamba ilisitisha safari yake ya Mwanza – Dar kuanzia juzi.
Â
Amesema katika ndege nne za ATCL (3-Bombardia na 1-Dreamliner), Bombardia zinaendelea na safari bila matatizo ila Dreamliner imesimamishwa kwa makusudi ili ifanyiwe matengenezo kwani kwa sasa ipo katika majaribio
Â
Marekebisho hayo ni kama ya WIFI na mengine madogo madogo yanayohusu uendeshaji wa ndege maana safari za ndege hiyo kwa sasa ni za majaribio kwa ndege yenyewe na Marubani pia.
Â
Aidha, amesema kuwa walipanga marekebisho hayo kufanyika wiki tatu baada ya kuanza safari zake, ila kilichopelekea marekebisho ya ghafla ni mafundi waliomba yafanyike mapema kwa kuwa wanaondoka nchini.
Â
-
Maafisa Madini wapewa somo utoaji wa leseni
Â
-
Video: Lissu narudi nyumbani, CCM waandamana kumpinga mbunge aliyeitosa Chadema
Â
-
DC Joketi: Sheria itachukua mkondo wake kwa atakaye kaidi agizo
Â
Hata hivyo, marekebisho hayo yaliyoanza juzi yanatarajiwa kukamilika leo na hivyo ndege hiyo kuanza safari zake kama kawaida hapo kesho.