Mzunguko wa raundi ya sita ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) unatarajiwa kuendelea kesho Jumamosi na Jumapili kwa timu 10 kucheza kusaka alama 3 muhimu.

Jijini Tanga Mgambo Shooting watakua wenyeji wa Coastal Union katika uwanja wa Mkwakwani, Majimaji FC watawakaribisha Mwadui FC uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Jumapili Stand United chama la wana watawakaribisha watoza ushuru wa jiji la Mbeya (Mbeya City) katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku Kagera Sugar wakiwa wenyeji wa Tanzania Prisons uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora na Toto Africa watakua wenyeji wa JKT Ruvu jijini Mwanza uwanja wa CCM Kirumba.

Chadema Yapanga Kulishitaki Jeshi La Polisi
Ligi Daraja la Kwanza Bara Kuendelea Kesho