Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Mathew, amepiga marufuku kumsainisha mwananchi mkataba kwa lugha za kigeni kwani yeyote anayefanya hivyo atakuwa na dhamira ovu dhidi ya mwananchi ndio maana anasainishwa mkataba kwa lugha asiyo ifahamu.

Amesema hayo wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi, uwezo na ubora wa minara ya mawasiliano, Wilayani Muheza Mkoani Tanga ambapo kusema kuwa Serikali itasimamia haki na maslahi ya wananchi kwa kuhakikisha wanasainishwa mikataba kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.

Amesema kuwa dhamira ya Wizara hiyo ni kuondoa migogoro ndani ya Sekta ya Mawasiliano kwa watoa huduma kufuata taratibu wakati wa ujenzi wa minara ikiwa ni pamoja na kupata vibali vinavyohitajika na kusaini mikataba na Serikali za vijiji kwa ajili ya ulinzi wa minara ya mawasiliano.

Mhandisi Kundo alitoa ametoa maagizo kwa watoa huduma kufanya malipo kupitia akaunti za benki kutoka kwenye kampuni kwenda moja kwa moja kwa walioingia nao mkataba ambao ni wamiliki wa maeneo waliyojenga minara ili kampuni kujiridhisha inamlipa mhusika na sio vinginevyo.

Aidha amezitaka taasisi mbili za mawasiliano ambazo ni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kuhakikisha wanakuja na majibu ya kupata suluhisho la kudumu tatizo la muingiliano wa mawasiliano katika maeneo yote ya mipaka nchini ifikapo tarehe 16/08/ 2021.

Aragija kupuliza kipyenga Fainali ASFC
Azam FC yamsajili Kenneth Muguna