Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Upendo Peneza ametoa mapendekezo yake kwa Serikali juu ya kukabiliana na Janga la Corona hasa katika kipindi hiki ambacho idadi ya wagonjwa inazidi kuongezeka zaidi ukilinganisha uwezo wa nchi kukabiliana na janga hilo akisema kuwa upo chini.

Peneza amesema kuwa katika kipindi hiki ni muhimu sana Serikali ifanye ushirikishwaji wa vitendo kufuatia tahadhari zinazotolewa hasa katika maeneo ambayo kuna wafanyabiashara mbalimbali kama vile wamama waliopo masokoni, gulio na maeneo ambayo watu wanafanya minada.

”Jitengeni kaeni mbali lakini Serikali haiwaambii na haiwasaidii ni namna gani ya kujipanga ili wakae mbali kwa kiasi hiko” amesema Peneza.

Amesema kuwa kufuatia janga hili wapo wafanyabaishara walioathirika pakubwa kama vile wamiliki wa shule pamoja na wafanyabaishara wa dhahabu, hivyo ameomba Serikali ione namna inavyoweza kuwasaidia walioathirika na Corona ili waweze kupata njia mbadala ya kujipatia mapato huku wakiendelea kujikinga na ugonjwa huo.

”Tufanye ushirikishwaji wa masuala ya biashara kuna watu wanaomiliki shule leo wamefunga shule hawana hela kuna masuala ya kikodi kuna watu wanaofanya biashara mbalimbali kama geita dhahabu saivi imekuwa ngumu kusafirisha dhahabu kwenda nje ya nchi imekuwa gharama kubwa wanalazimika kutoa mpaka ten thousand US Dolloars kusafirisha mzigo mdogo” Amesema Peneza.

Aidha ameomba iendelee kuwashirikisha wananchi ili waweze kutambua Changamoto walizonazo wafanyabiashara ambazo zitaathiri kodi na mapato ili waweze kuona wanasaidikaje na waweze kutengenezewa mazingira rafiki ya biashara zao.





Pia tushirikishe wananchi tutambue changamoto walizonazo za kibiashara
ambazo zinaenda kathiri kodi na mapato yao na tujue tunawasaiodiaje ka ili
tuwatengenezee mazingitera rafiki.





Pia tushirikishe wananchi tutambue changamoto walizonazo za kibiashara
ambazo zinaenda kathiri kodi na mapato yao na tujue tunawasaiodiaje ka ili
tuwatengenezee mazingitera rafiki.





Pia tushirikishe wananchi tutambue changamoto walizonazo za kibiashara
ambazo zinaenda kathiri kodi na mapato yao na tujue tunawasaiodiaje ka ili
tuwatengenezee mazingitera rafiki.





Pia tushirikishe wananchi tutambue changamoto walizonazo za kibiashara
ambazo zinaenda kathiri kodi na mapato yao na tujue tunawasaiodiaje ka ili
tuwatengenezee mazingitera rafiki.





Pia tushirikishe wananchi tutambue changamoto walizonazo za kibiashara
ambazo zinaenda kathiri kodi na mapato yao na tujue tunawasaiodiaje ka ili
tuwatengenezee mazingitera rafiki.





Pia tushirikishe wananchi tutambue changamoto walizonazo za kibiashara
ambazo zinaenda kathiri kodi na mapato yao na tujue tunawasaiodiaje ka ili
tuwatengenezee mazingitera rafiki.





Pia tushirikishe wananchi tutambue changamoto walizonazo za kibiashara
ambazo zinaenda kathiri kodi na mapato yao na tujue tunawasaiodiaje ka ili
tuwatengenezee mazingitera rafiki.

Watu wa Dar es salaam wasiruhusiwe kwenda maeneo mengine
Paul Nonga aiweka njiapanda Lipuli FC