Rais wa klabu ya Real Madrid, Florentino Pérez Rodríguez amefanikiwa kufanya mazungumzo na beki wa kati kutoka nchini Hispania, Sergio Ramos García ambaye alikua mbioni kuihama klabu hiyo kutokana na sakata la kupewa mkataba ambao hakuridhishwa nao.

Perez, alilazimika kusafiri hadi nchini China mwishoni mwa juma lililopita kwa ajili ya kufanya mazungumzo na beki huyo, na taarifa zinadai kwamba tayari wawili hao wameelewana na wakati wowote Ramos atasaini mkataba mnono ambao utaendelea kumuweka Estadio Santiago Bernabeu.

Taarifa zinasema kwamba mkataba mpya ulioandaliwa na uongozi wa klabu ya Real Madrid, dhidi ya beki huyo mwenye umri wa miaka 29 utajumuisha donge nono la Paund milion 10 ambalo ni sawa na Euro milion 13.5 ambazo zitamuwezesha kulipwa mshahara wake wa paund 260,000 kwa juma.

TAKUKURU Yamhoji Mwigulu Nchemba Tuhuma Za Rushwa
Watoto Wa Abedi Pele Wakamilisha Ndoto Zao