Muigizaji na muimbaji wa Bongo Flava, Meninah Ladiva amefunga ndoa mpya ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kufunga ndoa na Peter Haule, Mtoto wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Haule alibadili dini ili aweze  kuishi na mrembo huyo ndani ya ndoa na akabatizwa jina la Abdulkareem, jina ambalo bado Meninah analitumia kwenye akaunti yake ya Instagram.

Maisha ya ndoa ya Haule na Meninah yalikuwa ya ukimya, ndoa hiyo ilipelekea Malkia huyo wa ‘Kakopi Kapesti’ kuachana na muziki kwa muda wote, lakini kishindo kimeangukia pabaya baada ya talaka yao kujulikana wakati anatambulisha ndoa yake mpya.

Kupitia Instagram, Meninah amepost picha ya tukio hilo na ujumbe mzuri kwa mumewe huyo mpya.

Hiyo inamaanisha kuwa ndoa yake na Peter Haule ‘imebaki story’. Haijulikani sababu ya kuvunjika kwa ndoa hiyo.

Rich Mavoko: Diamond hakuniomba, Sikumuomba kuingia WCB
CUF watangaza kuziba nafasi ya Lipumba na Duni