Rais Samia Suluhu Hassan ashiriki Maadhimisho ya Miaka 62 ya Uhuru pamoja na Mchakato wa ukusanyaji maoni kutoka kwa wananchi kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Zifuatazo ni picha za matukio tofauti wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma hii leo Desemba 9, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Miaka 62 ya Uhuru na Mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, Makamu
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Lawrence Mafuru.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Lawrence Mafuru kuhusu kazi mbalimbali ambazo zinafanyika katika Tume hiyo wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Desemba 9, 2023. Maadhimisho hayo pamoja na uzinduzi wa Mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, yamefanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Msajili wa Hazina
Bw. Nehemia Mchechu mara baada ya kuwasili katika Banda la Maonesho la Hazina wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, Katibu Mtendaji
wa Tume ya Mipango, Lawrence Mafuru pamoja na baadhi ya Watumishi wa Tume hiyo na Wajumbe wa Bodi wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru pamoja na Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri
Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Lawrence Mafuru pamoja Makamishna wa Tume ya Mipango wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara pamoja na Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma Desemba 9, 2023.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru pamoja na uzinduzi wa Mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Maadhimisho hayo
yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

EAC iunge mkono jitihada za Wajasiriamali wadogo
Ukatili: Waathirika wa Ukoma wavunja ukimya