Makambako mji mdogo uliopo mkoani Njombe, asubuhi ya leo Askari polisi ajulikanae kwa jina la Zakayo Dotto Kileka amempiga risasi na kumsababishia kifo mpenzi wake ambae ni mwanajeshi anayejulikana kwa jina la Neema.

Mdogo wa marehemu ambaye alikua akiishi nae ameeleza kuwa Zakayo alimfumania dada yake Neema akiwa amelala na mwanaume mwingine na ugomvi mkubwa ulitokea baada ya kuona kazidiwa, Zakayo aliamua kutumia silaha.

‘’Jamaa alikimbia kwa hasira akaamua kumtwanga risasi mchumba wake’’ amesema mdogo wa Marehemu.

Hata hivyo katika harakati za kumsaka mtuhumiwa huyo, Pc Zakayo amejisalimisha kituo cha polisi Makambako asubuhi leo majira ya saa moja na nusu.

Alionekana katika vazi lake la uniform likiwa limelowa damu, lakini pia koromeo lake lameonekana kama mtu alietaka kujizuru.

Neema alikua akifanya kazi JWTZ Camp ya Makambako na Zakayo akiwa ni  Polisi Makambako katika ofisi za banki ya NMB.

Mwili wa marehemu Neema umehifadhiwa katika hospitali teule ya Ilembula baada ya kufanyiwa Pm katika hospitali ya mji Makambako. Neema ataagwa leo tayari kwa kuurejesha mwili makwao kwa maziko..

LUkuvi: Utambuzi wa umiliki wa maeneo na urasimishaji ni endelevu kwa mikoa yote nchini
Video: Tundu Lissu huenda akakaa hospitali miezi sita zaidi