Idara ya polisi mjini Los Angeles tayari imetoa jina la mshukiwa mmoja Eric Holder ambaye anatuhumiwa kuhusika kufyatua risasi na kumuua rapa Nipsey Husstle.

Ingawa Mamlaka zimesema bado zinamtafuta Holder, mkazi wa Los Angeles ambaye mara ya mwisho alionekana akikimbia eneo hilo lililofanyika shambulio la risasi mnamo Jumapili.

Hussle, mwenye umri wa miaka 33, aliuawa nje ya duka lake la Kusini Los Angeles, mavazi ya Marathon, siku ya Jumapili alasiri.

Jumatatu jioni, mamia walikuwa wamekusanyika nje ya duka, wakifunga barabara huku wakiwasha mishumaa ya flickering, maua na balloons.

Aidha shambulio lake hadi kifo chanzo kimetajwa kuwa ni kutokana na makala aliyokuwa akitaka kuiachia hivi karibuni inayohusisha dawa ya kuponya Virusi vya Ukimwi, hivyo kuuawa kwake ni kama njia mojawapo ya kurudisha nyuma makala hiyo yenye lengo la kuokoa mamia ya wanadamu duniani.

Japokuwa makala hayo hayajaungwa mkono kutokana na pesa nyingi inayoingia kwa serikali ya Marekani kutokana na biashara ya uuzaji dawa za Ukimwi zinazo punguza makali ya ugonjwa huo.

 

 

Wabunge wasusa watoka nje kupinga adhabu ya Halima Mdee
Nick Cannon kuendeleza alichokiacha Nipsey Hussle