Raia zaidi wanatarajiwa kuondolewa mapema hii leo kutoka mji unaoshikiliwa na waasi wa Darayya uliopo kwenye vitongoji vya mji mkuu wa Syria Damascus.
Watu hao wanapelekwa kwenye makao yaliyopo maeneo yanayoshikiliwa na majeshi ya serikali mjini humo.
Aidha Mwandishi wa BBC eneo hilo amesema kwa kuna wasiwasi kwamba raia walioshirika maandamano ya kuipinga serikali ya rais Assad huenda wakateswa.na Umoja wa mataifa umesema kuwa kuhamishwa kwa raia hao kunastahili kuwe ni hiari ya mtu na si lazima.