Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Kipa wa Young Africans na timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Deogratius Munishi kutokana na kifo cha Baba yake mzazi, Mzee Boniventur Munishi kilichotokea jana Agosti 28, 2016.

Rais Malinzi amepokea taarifa za kifo cha Mzee Boniventur Munishi mara baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) Young Africans na African Lyon uliofanyika jana Agosti 28, 2016 ambako Deogratius aliongoza timu yake Young Africans kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 bila kufahamu kuwa amepoteza baba.

“Ni ujasiri wa aina yake aliokuwa nao Kipa Munishi kwenye mchezo wa Ligi Kuu bila kuonyesha tofauti,” amesema Malinzi ambaye katika zake za rambirambi kwenda kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki amewataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa mpendwa wao.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Mzee Boniventur Munishi mahala pema peponi.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe.

 

Lema ashtakiwa kwa kumtumia ujumbe huu wa simu Mkuu wa Mkoa Arusha
Mchezo Wa Yanga SC Vs Ruvu JKT Waahirishwa