Kipa wa zamani wa Azam Fc, Razak Abalora amesajiliwa na klabu ya Asante Kotoko ya nchini Ghana na hii imekuja baada tu ya jana kuingoza vizuri timu ya taifa hilo ( GHANA ), kupata ushindi wa mabao 5 – 1 dhidi ya QATAR, yeye akiwa langoni.

Abalora ana umri wa miaka 24 na aliitwa timu ya Taifa akiwa hana timu, baada ya kuachwa na Azam Fc aliyoitumikia kwa miaka mitatu.

Mwandishi wa habari za michezo nchini Ghana, Myk Alonso anamtaja Abalora kama kipa anayetarajiwa kuwa tegemeo zaidi ktk timu ya Taifa kwa siku zijazo.

mvua za vuli kuendelea kunyesha Dar
Prince Dube kulekea mchezo wa kesho dhidi ya Mwadui