Ripoti ya Taasisi ya Kuchunguza Makosa ya Ufisadi (SFO) ya Uingereza imewataja mawaziri wawili wa serikali ya awamu ya nne kuwa walihusika katika ufisadi wa zaidi ya bilioni 13.

Ufisadi huo ulifanyika wakati serikali ya Tanzania ilipokopa Dola za Kimarekani 600 (shilingi trilioni 1.3) kupitia benki ya Standard ya Uingereza.

Baadhi ya watumishi wa Benki ya Stanbic wametajwa kuhusika kuongeza asilimia moja ya mkopo huo (kati ya shilingi bilioni 13 na 15)wakishirikiana na waliokuwa watumishi wa serikali kati ya mwaka 2012 na 2013.

Ripoti hiyo iliyowasilishwa katika mahakama ya Southwark Crown ya Afrika Kusini, imewataja mawaziri wawili wa fedha wa zamani, Mustafa Mkulo na Dk. William Mgimwa ambaye ni marehemu.

Mawaziri hao wanatajwa kuhusika kusaidia udanganyifu huo wakishirikiana na watumishi wengine wa umma.

Wengine waliotajwa kwenye sakata hilo ni pamona na aliyekuwa Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitillya. Kwa upande wa Stanbic Bank tawi la Tanzania, waliotajwa kuhusika ni Bashir Awale na Shose Sinare (Miss Tanzania 1996).

Uongozi wa Chadema wazungumzia Kasi ya Magufuli
Kocha Wa Yanga Afanya Maamuzi Magumu