Mwanasheria wa aliyekuwa Rais wa shirikisho la Soka Duniani FIFA Sepp Blatter anatarajiwa kuwasilisha rufaa yake kupinga kufungiwa miaka minane kujishughulisha na masuala ya soka.

Hata hivyo kamati ya nidhamu ya FIFA imewasilisha sababu za kuchukuliwa kwa hatua za nidhamu dhidi ya viongozi hao waandamizi wa zamani wa soka Blatter na mwenzake, Michel Platini.

Mwezi Disemba aliyekuwa Rais wa FIFA Sepp Blatter na rais wa UEFA Michel Platini walifungia kwa kipindi cha miaka minane baada ya kukutwa na hatia ya kuvunja kanuni na sharia za FIFA.

Kwa upande wake pia mwanasheria wa Platini anasema kuwa anatarajia kukata rufaa kwa kupinga maamuzi ya FIFA.

Man City Yabisha Hodi Ujerumani
Maalim Seif Kutoa Siri ya Mazungumzo ya Kusaka Maridhiano Zanzibar, Leo