Serikali ya Sudan na makundi ya waasi leo yametia saini mkataba wa kihsitoria wa amani unaolenga kumaliza miongo kadhaa ya vita vilivyohujumu maisha ya mamia kwa maelfu ya watu.

Kulikuwa na shamra shamra wakati wawakilishi wa serikali na makundi ya waasi walipotia saini hati ya mkataba huo ikiwa ni takriban mwaka mmoja tangu kuanza kwa mazungumzo ya kusaka amani baina ya pande hizo.

Hafla ya kutia saini imefanyika kwenye mji mkuu wa taifa jirani la Sudan Kusini, Juba, na kuhudhuriwa na wawakilishi wa Chad, Qatar, Mirsi, Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya na Umoja wa Mataifa.

Mkataba huo unajumuisha masuala kadhaa ikiwemo umiliki ardhi, mgawanyo wa madaraka na mapato ya serikali na kurejea kwa wakimbizi na raia waliopoteza makaazi wakati wote wa mzozo.

Aidha, chini ya hati ya makubaliano, wapiganaji wa makundi ya waasi kutoka majimbo ya Darfur, Kordofan ya Kusini na Blue Nile watajumuishwa taratibu kwenye vikosi vya jeshi la serikali.

Habari kubwa kwenye magazeti leo, Oktoba 5, 2020
Jela miaka 7 kwa kutumia jina la waziri mkuu