Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa amewataka wahitimu wa Chuo cha Afya K’S  kilichopo  Jiji la Mbeya, kwenda kuitumikia Jamii kwa uzalendo na Upendo kwani  Serikali imewekeza kwenye Huduma bora za Afya Nchini.

Akizungumza kwenye Mahafali ya nane ya Chuo hicho, Malisa  amewakumbusha wajibu wao kama Wataalam wa Afya kuwa, jamii inawahitaji  hivyo ni vyema kutumia lugha za upendo katika kuwahudumia wagonjwa.

Kwa Upande wake, Mkuu  wa chuo hicho, Norbert Sizari ameishukuru  Serikali kupitia Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa ushirikiano wa na kuwapatia Wanafunzi fursa ya  mafunzo kwa Vitendo.

Mapema wiki hii, Serikali pia iliwataka Wauguzi wa kada ya Utabibu, Wakunga na Wauguzi nchini, kutumia mitandao ya kijamii vizuri bila kwenda kinyume na maadili ya fani yao, na kuacha kutumia lugha chafu na kejeli kwa wagonjwa ili kuheshimisha kada hiyo.

Pochettino ataka kiungo mzoefu
Tanga yatarajia kuzalisha Wanasayansi Mahiri Kitaifa