Waziri kivuli wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, na Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la (Sugu) ameitaka Serikali kuacha mara moja mwenendo wa kutisha, kushambulia na kudhibiti uhuru wa vyombo vya habari.

Sugu ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia tiketi ya Chadema, amesema kuwa kufungiwa kwa magazeti na baadhi ya vyombo vya habari ni vitisho ambavyo vinadidimiza uhuru wa habari.

Amesema kuwa uamuzi wa serikali wa kuvifungia baadhi ya vyombo habari ni kwenda kinyume na misingi ya utoaji haki ya utoaji wa habari, ambapo kunaiathiri kwa kiasi kikubwa jamii ambayo ndiyo mlaji mkuu wa habari.

Aidha, ameongeza kuwa kifungu cha 51(1) cha sheria hiyo inayotumiwa na serikali kufungia baadhi ya vyombo vya habari, hakitoi mamlaka yeyote kwa serikali kuchukua hatua dhidi ya chombo cha habari.

Video: Mvua yaleta kizaazaa, Barrick yaweka masharti malipo ya sh700 bilioni
Trump aanika nyaraka za upelelezi wa mauaji ya ‘Rais Kennedy’