Jumla ya waamuzi chipukizi 29 wasiokua na beji za FIFA kutoka nchi 28 barani Afrika wanatarajiwa kuhudhuria kozi ya waamuzi inayoandaliwa na FIFA kwa kushirikiana na CAF itakayofanyika kuanzia kesho Jumamosi tarehe 26 –30 Septemba mwaka huu jijini Dra es salaam.

Kozi hiyo itaendeshwa na wakufunzi kutoka katika nchi za Afrika Kusini, Malawi, Misri na Mauritius itafanyika katika hoteli ya Holiday Inn iliyopo jijini Dar es salaam ambapo waamuzi chipukizi kutoka Tanzania watakohudhuria ni Abdallah Kambuzi (Shinyanga) na Shomari Lawi (Kigoma).

Lengo la kozi hiyo ni kuwaanda waamuzi wanaochipukia ili baadae kuweza kuwa waamuzi wa FIFA ambao watatumika kwa michuano mbalimbali.

Utafiti Mwingine Wa Septemba Wampa Lowassa Ushindi
SSC Napoli Kumsaidia Jese Rodriguez Wa Real Madrid