Washika Bunduki wa kaskazini mwa London Arsenal FC wako kwenye mazungumzo ya kumtoa kwa mkopo kiungo wao wa kati Matteo Guendouzi kwenda Olympic Marseille.

Wakati huo huo Arsenal wameongeza jitihada za kumshawishi kiungo wa kati anayekipiga Olympic Lyon Houssem Aouar mwenye umri wa miaka 22, huku rais wa klabu hiyo ya Ufaransa Jean- Michel Aulas akikiri kuwa wanaweza kuwapoteza wachezaji wawili kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.

  • Klabu ya Tottenham imefikia makubaliano ya kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Benfica Carlos Vinicius mwenye umri wa miaka 25,  ambaye ada yake ya usajili ni Pauni milioni 89 kwa mujibu wa kufungu cha mkataba wake.
  • Wakala wa Mshambuliaji wa Real Madrid Luka Jovic mwenye umri wa miaka 22, amesema mchezaji huyo kutoka nchini Serbia anataka kujiunga na Manchester United, huku inter Milan na AS Roma zote za Italia, zikionyesha nia ya kumsajili.
  • Mabingwa wa soka nchini England Liverpool wanajiandaa kukubali ofa ya Pauni Milioni 23 kutoka Sheffield United kwa ajili ya mshambuliaji Rhian Brewster.
  • Newcastle United wanajiandaa kupambana na Valencia katika mbio za kumsajili mlinzi wa Juventus Daniele Rugani ambaye pia anahusishwa na taarifa za kuwaniwa na klabu za Fulham, West Ham (England) na Sevilla (Hispania).
  • Klabu ya Aston villa ipo mbioni kumsajili beki wa kati Kerr Smith mwenye umri wa miaka 15, kutoka Dundee United.

Mauaji ya wazee yapungua
Makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya kupangwa leo