Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za rambi rambi kwa klabu ya Tanzania Prisons inayoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom kufuatia kifo cha Mwenyekiti wake Hassan Mlilo kilichotokea jana katika hospital ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam.

Katika salamu zake, Malinzi amewapa pole familia ya marehemu Hassan Mlilo, ndugu, jamaa, marafiki na klabu ya Tanzania Prisons, na kusema kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini amesema TFF ipo pamoja nao katika kipindi hichi kigumu cha maombolezo.

Mwili wa marehemu Hassan Mlilo unatarajiwa kusafirishwa leo mchana kuelekea mkoani Mbeya, ambapo mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho katika mji wa Rujewa mkoani humo.

Kombe La Shirikisho Lafikia Patamu, Vigogo Kuanza Kesho
My Story: Alichonifanya huyu mrembo kwenye daladala kinaniuguza