Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima ameagiza kusimamishwa kazi Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Chunya, Dkt Felista Kisandu, kwa kukiuka mwongozo wa utoaji wa taarifa za milipuko kama ilivyoelezwa kwenye Sheria ya Afya ya Umma (Public Health Act) ya mwaka 2009.

Akitoa tamko hilo February 7 2021 Dkt. Gwajima amesema Dkt. Kisandu anapisha uchunguzi kufuatia sakata la kusambaa kwa taarifa ya mlipuko wa ugonjwa usiofahamika kata ya Ifumbo wilayani Chunya.

“Kutokana na kadhia hii ambayo imeleta taharuki isiyo ya lazima naiagiza mamlaka ya ajira ya Dkt. Felista Kisandu ambaye ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Chunya ichukue hatua za kumsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi chini ya Baraza la Madaktari na taarifa nipate ndani ya siku 10,” amesema Dkt Gwajima.

Amesema katika Kata ya Ifumbo, Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya hakuna mlipuko wa ugonjwa wowote uliothibitishwa wala hakuna janga lolote la kiafya kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari.

Aidha amesema timu ya wataalamu imefanya mahojiano na wananchi na kubaini hakuna vifo 15 kwa mara moja vya wagonjwa wanaodaiwa kuwa na dalili za kutapika damu kama ilivyoripotiwa na diwani wa Kata ya Ifumbo na takwimu hizo hazijawahi kuripotiwa popote.

Kigonya asimulia penati ya Chama
Habari kubwa kwenye magazeti leo, Februari 8, 2021