Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi  amesema ushirikiano wa kisekta katika ufanyaji kazi ni jambo zuri linaloleta ufanisi na ubora katika kazi zinazokuza uchumi wa Taifa.

Dkt. Yonaz ameyasema hayo baada ya kutembelea na kukagua miradi ya kimkakati iliyoko visiwani Zanzibar, ukiwemo wa Bandari Jumuishi wa Manga Pwani, Nyumba za Makazi na Biashara pamoja na mradi wa nyumba za gharama nafuu.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi akizungumza wakati wa Majumuisho ya Ziara ya kujifunza utendaji kazi wa Idara ya Ufutiliaji na Tathmini ya Tume ya Mipango Zanzibar.

Amesema, “Taasisi zetu zitaendelea kufanya kazi kwa pamoja ili kutengeneza Uchumi imara katika eneo letu la Afrika Mashariki na Kati, na tukitambua kwamba soko letu linazidi kukua lakini sisi kama Nchi pia tuna fursa katika soko la SADEC, kwa hiyo tukizingatie tunapakana na nchi nyingi hivyo tukitumia vizuri tunayo nafasi ya kujenga uchumi.”

Aidha, Dkt. Yonazi ameongeza kuwa Serikali imefanya uamuzi kuanzisha kurugenzi za Ufuatiliaji na Tathmini  katika kila Wizara ambapo itasaidia Serikali kufuatilia miradi yake ,mipango yake na  kufaya maamuzi ya kiutendaji kwa wakati.

Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar Dkt. Rahma Salim Mahfoudh akieleza namna ya Tume hiyo inavyofanya kazi.

Kwa upande wake  Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar, Dkt. Rahma Salim Mahfoudh amesema jukumu la msingi la Ufuatiliaji na Tathmini Zanzibar ni kupanga na kufuatilia miradi ambapo kwa sasa wanampango wa muda wa kati wa mwaka 2021 na 2026.

“Tuna miradi ya Kimkakati ambayo tunapoifanya inaongeza ufanisi katika kazi yetu na katika Miradi mliyotembelea leo ni Miradi ya kimkakati ya Nchi ambayo tunawapa sapoti kwa asilimia mia moja hasa  kwa mradi kama shirika la nyumba ni fedha za serikali ambazo zimeingizwa ili kuufanya mradi ule,” alisema Katibu Mtendaji.

Baadhi ya Viongozi na Maafisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu wakati wa ziara Kukagua Miradi ya Kimkakati iliyoko Visiani Zazibar.

Viongozi na Maafisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu wako visiwani Zanzibar kwa ziara ya siku mbili ya kujifunza  utendaji kazi wa  Idara ya Ufutiliaji na Tathmini ya Tume ya Mipango Zanzibar.

Wasanii wapewa darasa mkopo wa Bil. 20 za Rais Samia
Chukwu afunguka mapungufu Singida FG