Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi leo Septemba 2, 2016 amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mwenge.
Hapi amewapongeza TRA na kuwataka wasibweteke badala yake wahakikishe wanakusanya kodi kwa watu wote.
Hapi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais, Magufuli katika vipaumbele vyake ni pamoja na kuhakikisha watu wanaostahili kulipa Kodi wanalipa kwa wakati kwa mujibu wa sheria na taratibu. Bofya hapa kutazama video #USIPITWE