Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto imetangaza kuendelea kuwapo kwa ugonjwa wa homa ya Dengi (Dengue) hususani katika majiji ya Dar es Salaam na Tanga kuanzia Januari 2019.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari wa Bunge jijini Dodoma amesema hadi kufikia aprili 2 mwaka huu kati ya watu 470 waliopimwa 307 wamethibitishwa kuwa na virusi au kupata ugonjwa huo kati yao 252 ni kutoka dar na 55 kutoka Tanga.

Mradi wa maji wamuweka kikaangoni mkurugenzi Makambako
Video: Mtenda kazi ndiye mleta kazi kama Rais Magufuli - Mwijage