Kocha wa mabingwa wa soka duniani timu ya taifa ya Ufaransa Didier Deschamps, amewalaumu wachezaji wake kwa kushinda kufikia lengo la kupata matokeo ya ushindi dhidi ya Ujerumani, katika mchezo wa michuano ya ligi ya mataifa ya Ulaya (UEFA Nations Leagua) uliocheza usiku wa kuamkia leo.

Miamba hiyo ya soka ilikutana mjini Munich katika mchezo wa kundi A wa michuano hiyo, inayofanyika kwa mara ya kwanza barani Ulaya na kushuhudia ikishindwa kufungana.

Kocha Deschamps aliwaambia waandishi wa habari baada ya mchezo huo kuwa, kikosi chake kilifanya makosa mengi ambayo yamewakosesha ushindi katika uwanja wa ugenini.

Alisema aliweka mipango mizuri kabla na wakati wa mapumziko ambayo aanaamini kama ingetumika vizuri, Ufaransa huenda wangeondoka ugenini na ushindi mzuri wa mabao.

“Sikupendezwa na walivyocheza, wameonyesha udhaifu mkubwa dhidi ya wapinzani wetu, hatukupaswa kupata matokeo ya bila kufungana,” Alisema kocha huyo mwenye umri wamiaka 49.

“Hawakufuata maelekezo niliyowapa kabla na wakati wa mapumziko, niliamini wangefanikisha hilo, lakini ilikua tofauti kabisa, matokeo yake tumeopata alama moja.”

“Lengo letu kubwa lilikua ni kupata ushindi katika mchezo huu ili tujiweke katika mazingira ya kuongoza msimamo wa kundi letu, lakini hatuna budi kukubaliana na matokeo yaliyopatikana, tutajipanga kwa mchezo unaofuata.”

Mchezo wa jana dhidi ya Ujerumani ulikuwa wa kwanza kwa kocha Deschamps baada ya kukamilisha jukumu la kutwaa ubingwa wa dunia nchini Urusi, kwa kuichapa Croatia mabao manne kwa mawili mwezi Julai.

Ufaransa watacheza mchezo wa mzunguuko wa pili wa kundi A Septemba 09, dhidi ya Uholanzi kwenye uwanja wa taifa mjini Paris (Stade de France).

Matokeo ya michezo mingine ya ligi ya mataifa ya Ulaya (UEFA Nationas League).

Kundi B

Jamuhiri ya Czech 1 – 2 Ukraine

Wales 4 – 1 Ireland

Kundi C

Norway 2 – 0 Cyprus

Slovenia 1 – 2 Bulgaria

Kundi D

Kazakhstan 0 – 2 Georgia

Latvia 0 – 0 Andorra

Kundi E.

Armenia2 – 1Liechtenstein

Gibraltar 0 – 2 FYR Macedonia

Michuano hiyo itaendelea tena hii leo .

Kundi A

Italy Vs Poland

Kundi B

Turkey Vs Russia

Kundi C

Albania Vs Israel

Lithuania Vs Serbia

Romania Vs Montenegro

Kundi D

Azerbaijan Vs Kosovo

Faroe Islands Vs Malta

Video: Mimi sikufukuzi mkurugenzi, chapa kazi- Rais Dkt. Magufuli
Habari kubwa katika magazeti ya Tanzania leo Septemba 7, 2018