Wazazi na walezi nchini  wametakiwa kuhimizana na kusambaza elimu kwa wale wanaokataa kutoa michango ya chakula shuleni.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa Kagera, Albert  Chalamila hivi karibuni Mkoani Kagera na kuongeza kuwa wengi wa wanaokataa kutoa  mchango huo hawana sababu za msingi.

Amesema, “wapo wazazi wamewapeleka watoto wao kwenye shule za kawaida na pengine bure kabisa ila ukimwambia mchango wa uji na chakula kwa mtoto wake maelezo yanakuwa mengi, sasa nendeni mkawe mabalozi wazuri huko.”

WFP yaonya mgogoro wa kibinadamu ukanda wa EA
Mkanganyiko kujiuzulu kwa Meja Jenerali Nyagaya