Mkurugenzi wa Bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB), Abdul Razaq Badru amesema kuwa bodi hiyo itafungua dirisha la kukata rufaa kwa wanafunzi waliokosa mikopo ili waweze kupata haki yao.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati akifafanua vigezo na sifa za mwanafunzi kupata mkopo baada ya kuwepo kwa kasoro kadhaa kwa baadhi ya waombaji katika awamu ya kwanza ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza.

“Kwa wale wenye changamoto ndogo ndogo labda walikosea, tutatangaza dirisha la kukata rufaa mapema wiki ijayo na tutashughulikia watakaokamilisha vigezo watapata mkopo lakini wanatakiwa kuzingatia maelekezo tutakayoyatoa,” amesema Badru

Hata hivyo, mkurugenzi amesema katika majina ya waombaji waliyoyapokea na kudhibitishwa na TCU kwamba yamepata vyuo na wakayapitia wakajiridhisha hayana kasoro kwenye uombaji, tayari wanafunzi 29,578 wameshapata mkopo na wameanza masomo ambapo kiasi cha shilingi bilioni 96 zimetumwa vyuoni.

Serikali kutenga trilioni 7.6 kulipa mishahara
Trump aanza ziara yake Korea Kusini