Idadi kubwa ya wanafunzi wa chuo kikuu wametekwa nyara kwenye shambulizi la watu wenye silaha lililoendeshwa katika jimbo la Abia, nchini Nigeria.

Kwa mujibu wa Kamishna wa Habari wa Jimbo la Abia, John Kalu watu wenye silaha walishambulia gari lililokuwa limebeba wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Jimbo la Abia (ABSU) kwenye barabara kuu ya jimbo la Okigwe-Uturu.

Kalu amesema kuwa wanafunzi wengi walitekwa nyara katika shambulizi hilo ambapo wanafunzi wengine wawili walifanikiwa kutoroka.

Akibainisha kwamba walishirikiana na vikosi vya usalama katika jimbo jirani la Imo kuwaokoa wanafunzi waliotekwa nyara, Kalu amesema, “Tunapendekeza umma na jamii ya ABSU ibaki na utulivu kwa sababu hatutatenga rasilimali yoyote kuhakikisha usalama wa wahanga.”

Katika majimbo ya Nigeria kama Benue, Plateau, Katsina na Zamfara, shule zilishambuliwa mara kadhaa tangu Januari na wanafunzi walitekwa nyara.

Wanafunzi 16 walitekwa nyara katika shambulizi la watu wenye silaha lililotekelezwa mnamo Aprili 20 kwenye Chuo Kikuu binafsi cha Green Field katika jimbo la Kaduna.

Shughuli za masomo zilisitishwa katika baadhi ya majimbo kwa sababu ya mashambulizi yaliyolenga shule nchini Nigeria.

Serikali yamkabidhi Kikwete nyumba ya kuishi
Wawili wafariki mgodini Mirerani