Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imetoa onyo kwa watu wanaowarubuni wananchi kupitia vitambulisho vya kupigia kura kwa kuwapa fedha na kuuza kadi hizo kwani wanawaondolea wananchi haki ya msingi ya kikatiba.

Akitolea taarifa juu ya jambo hilo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Afisa Uhusiano wa TAKUKURU, Doreen Kapwani amewataka wanaojihusisha na vitendo hivyo waache mara moja kwani wakikamatwa watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani.

Mwanafunzi aliyemjeruhi mwalimu afikishwa mahakamani, akosa dhamana
Tuzo za BET zamuibua Octopizzo