Gwiji wa Manchester United Wayne Rooney amesema anaamini Marcus Rashford ndiye mchezaji pekee katika klabu hiyo ambaye anaweza kumpita kama mfungaji bora wa muda wote, lakini akasema anamhurumia kwa kuanza msimu kwa ugumu.

Rashford alifunga mabao 30 katika michuano yote msimu uliopita, lakini ameifungia United mabao saba pekee kwenye kampeni hiyo.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26, alipigwa faini na kuachwa nje ya ushindi wa United wa Kombe la FA raundi ya nne dhidi ya Newport County mwezi uliopita baada ya kujirusha kwenye klabu ya usiku ya Belfast wakati akidai kwamba alikuwa mgonjwa.

Akizungumza na TNT Sports Rooney alisema: “Rashford yupo katika nafasi ya upendeleo ambapo anachezea Manchester United.

“Nilishasema hapo awali, ndiye mchezaji mmoja ambaye niliamini kabisa angeweza kwenda kupata rekodi yangu ya ufungaji na natumai atafanya hivyo kwa sababu ni kijana wa Manchester, lakini anahitaji kuwa na uthabiti.

“Kwa kweli, hana msimu bora zaidi, lakini anahitaji kupata kiwango na uthabiti na kuwa kiongozi wa timu hii.”

Ancelotti: Vinicius Jr anatendewa sivyo

Rooney alifunga mabao 253 kwenye mechi 559 katika kipindi cha miaka 13 akiwa United, huku Rashford akiwa na nusu ya jumla ya mabao hayo.

TanTrade yajadili matokeo utafiti hali ya Biashara Nchini
Thomas Frank alia na udanganyifu