Kocha Mkuu wa Arsenal Mikel Arteta amesema kikosi chake kipo tayari kuipa changamoto Manchester City hadi siku ya mwisho ya msimu, lakini akawaonya wachezaji wake kusahau ushindi wa mabao 3-2 wa Jumapili (Aprili 28) dhidi ya Tottenham Hotspur.

Arsenal walipata mabao yao kupitia kwa Pierre Emile Hojbjerg bao la kujifunga pamoja na mabao ya Bukayo Saka na Kai Havertz.

Alipoulizwa kabla ya City kuifunga Nottingham Forest baadaye kama ushindi huo ulikuwa ushahidi kwamba kikosi chake kiko tayari kupambana hadi mwisho, Arteta, ambaye alipata ushindi wake wa 100 wa ligi kama kocha alisema: “Ndio, asilimia 100 kwa msimu mzima.

“Wananipa sababu ya kuamini kwamba kila siku tuko sawa.  Motisha ya kile kilicho mbele ni nzuri. Sote tunatarajia kwamba tutakwenda kweli.”

Arsenal ilianguka ilipoongoza mbio za ubingwa mwaka jana mwanzoni mwa Aprili, lakini sasa imepata ushindi mara tatu mfululizo wa ligi baada ya kutoka kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya katika hatua ya Robo Fainali dhidi ya Bayern Munich.  Kwa sasa wamekaa kwa pointi moja mbele ya City, ambao wana mchezo mmoja mkononi.

“Mwisho hukumu itategemea matokeo,” Arteta alisema.

“Kama wangepata bao dakika za mwisho na kufanya matokeo kuwa 3-3, basi tusingekuwa tayari kushinda ligi. Tunataka kuwa bora zaidi. Kuna tofauti za kuboresha. Tutakwenda tena dhidi ya Bournemouth Jumamosi na itakuwa ngumu sana.”

Serikali kuunda timu tatu AFCON 2027
Ombi la USM Alger limegonga mwamba