Bendera ya Taifa la Finland inatarajiwa kuinuliwa katika makao makuu ya Nato huko Brussels, kuashiria kuwa mwanachama wa 31 wa muungano wa nchi za Magharibi.

Kujiunga kwa Finland ni kikwazo kwa Vladimir Putin wa Urusi, ambaye alilalamika mara kwa mara juu ya upanuzi wa Nato kabla ya uvamizi wake Ukraine.

Finland ina sehemu ya mpaka wa mashariki wa kilomita 1,340 (maili 832) na Urusi na iliomba rasmi kujiunga na muungano wa usalama wa Magharibi Mei 2022 kwa sababu ya vita vya Urusi.

Bendera ya Finland

Hapo awali wote wawili walikuwa wamepitisha sera ya kutofungamana na upande wowote. Lakini mbele ya jeshi la Urusi walipendelea kuhamia dhamana ya ulinzi iliyotolewa na kifungu cha tano cha Nato, ambacho kinasema kuwa shambulio dhidi ya mwanachama mmoja ni shambulio la wote.

Ombi la Sweden kwa sasa limekwama, huku Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akiishutumu Stockholm kwa kuwakumbatia wanamgambo wa Kikurdi na kuwaruhusu kuandamana mitaani. Hungary pia bado haijaidhinisha Sweden kujiunga.

Salah anavyouheshimu mwezi mtukufu
Jean Baleke: Tuna kazi kubwa mbele yetu